LAGOS, Nigeria
STAA wa Afrobeat, Wizkid, amemjibu mkongwe wa muziki huo, 2Baba, akimwita ‘babu’ kutokana na maoni yake ya hivi karibuni.
2Baba aliulizwa maoni yake juu ya nani mkali wa Afrobeat kati ya mastaa watatu wa Nigeria; Wizkid, Davido na Burna Boy.
Akijibu swali hilo, licha ya kukubali uwezo wa kila mmoja, 2Baba aliyewahi kutamba na ‘African Queens’, alimtaja Burna Boy.
Jibu hilo sasa limemchonganisha na Wizkid, ambaye ametumia kurasa zake za mitandao ya kijamii kumtolea uvivu 2Baba.
Wizkid ameenda mbali zaidi na kumtaka 2Baba kushughulikia changamoto zake za kifamilia, badala ya kutoa maoni kwenye soko la muziki.no wa Tanzania, Kenya na Uganda.


