NEW YORK, Marekani
STAA wa muziki wa Hip hop, Sean Combs ‘P. Diddy’, amekwaa kisiki katika kesi zinazomkabili baada ya juzi kunyimwa dhamana.
P. Diddy anasota gerezani akikabiliwa na mashitaka mbalimbali, yakiwamo ya udhalilishaji wa dhidi ya wasichana aliokuwa akiwasafirisha maeneo mbalimbali kwa ajili ya biashara ya ngono.
Kwa kukosa dhamana, sasa rapa huyo ambaye anashikiliwa tangu Septemba, mwaka jana, atalazimika kubaki gerezani hadi hukumu yake itakaposomwa.
Endapo msanii huyo atakutwa na hatia, basi atashukiwa na adhabu ya kifungo cha miaka 20 gerezani.
P. Diddy akwaa kisiki, arudishwa gerezani
Published:


