LILLE, Ufaransa
STAA wa zamani wa Chelsea, Eden Hazard, ameeleza kushangazwa na namna Olivier Giroud anavyoendelea kucheza kwa kiwango cha juu, licha ya umri wake mkubwa wa miaka 38.
Hazard raia wa Ubelgiji, amezidiwa miaka minne na Giroud lakini alishastaafu soka, jambo ambalo ameeleza kuwa linaendelea kumshangaza.
Giroud alijiunga na Lille hivi karibuni baada ya kuachana na Los Angeles FC. Vigogo hao wa Ufaransa wamempa mkataba wa mwaka mmoja.
Hazard ni mmoja ya wachezaji wenye heshima kubwa katika klabu ya Lille, akikumbukwa na mashabiki wake kwa mabao 50 na kuipa taji la Ligue 1 mwaka 2011.
Hazard amshangaa Giroud
Published:


