33.3 C
New York

Yanga, Simba katikati ya Mamelodi inayosaka rekodi CAF

Published:

Na mwandishi wetu, Gazetini

SHIRIKISHO la Soka barani Afrika (CAF) hivi karibuni lilianika kalenda ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa msimu ujao wa 2026-27, ukiwa ni wa 63 tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo.

Kutokana na viwango vya CAF kwa miaka mitano iliyopita, nchi 12 zina tiketi mbili za uwakilishi kwenye mashindano hayo.

Nchi hizo ni Misri, Morocco, Algeria, Afrika Kusini, Tanzania, Tunisia, Angola, DRC, Sudan, Mali, Ivory Coast na Nigeria.

TIMU HIZI HAPA

Afrika Kusini itawakilishwa na Mamelodi Sundowns na Orlando Pirates, Misri ina Zamalek na Pyramids FC, wakati Morocco inawakilishwa na AS FAR na Wydad Casablanca.

Timu zingine ni Esperance Tunis na Club Africain (Tunisia), Enugu Rangers na Rivers United (Nigeria), Williet (Angola), ASEC Mimosas na San Pedro (Ivory Coast).

Pia, kuna hizi; Simba na Yanga (Tanzania), Gor Mahia (Kenya), Power Dynamos (Zambia), Scottland (Zimbabwe) na Medeama (Ghana).

Ikumbukwe kuwa bingwa wa msimu ujao wa mashindano hayo atajiondokea na kitita cha Dola za Marekani milioni 6.

AL AHLY CHALI

Kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2003, vigogo wa soka la Afrika, Al Ahly, watana Petro Atletico na wataikosa Ligi ya Mabingwa msimu ujao wa 2026-27.

Al Ahly, mabingwa mara nyingi zaidi katika historia ya michuano hiyo, walishindwa kufuzu baada ya kumaliza nyuma ya Zamalek na Pyramids msimu uliomalizika (2025-26) wa Ligi Kuu ya Misri.

Wakati Al Ahly wakiugulia mujibu hayo, Williet ya Angola itakuwa inasherehekea kutia mguu kwa mara ya kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika.

MAMELODI TENA?

Baada ya ubingwa msimu wa 2025-26, Mamelodi Sundowns watarejea kujaribu kulitetea taji lao. Je, itakuwa timu ya kwanza ya Afrika Kusini kubeba mara mbili mfululizo?

Wapinzani wao kwenye soka la ndani, Orlando Pirates, nao wamepata tiketi ya uwakilishi baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Afrika Kusini msimu wa 2025-26.

RATIBA KAMILI

Kama ilivyo kawaida, timu zitaanzia hatua ya awali, kisha kuingia raundi ya kwanza itakayochezwa kati ya Septemba 4-6, 2026.

Baada ya matokeo ya raundi ya pili itakayochezwa kati ya Oktoba 16-18, 2026, timu 16 zitaingia hatua ya makundi.

Mechi za hatua ya makundi zitachezwa kati ya Novemba 27-29, 2026. Kila timu itachezwa mechi zake tatu kabla ya Krismasi, kisha zitarudiana kati ya Januari 8-10, 2027.

Hatua hiyo itatamatika kwa kubakiza timu nane zitakaoingia robo fainali itakayoanza kuchezwa kati ya Februari 26-28, 2027.

Michezo ya marudiano itachezwa wiki moja baadaye, kisha nusu fainali itapigwa kati ya Aprili 9-16, kabla ya fainali ya Mei 9, 2027.

Related articles

Recent articles