Na mwandishi wetu, Gazetini
MWENYEKITI wa klabu ya Simba, Murtaza Mangungu, amekanusha taarifa za kuwapo kwa mgogoro kati ya viongozi, akisema ni upotoshaji unaifanywa kwa lengo la kuwagawa.
Mangungu ameyasema hayo Desemba 19, 2025, katika Mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Kwa muda sasa, zimekuwapo taarifa za mvutano miongoni mwa viongozi wa Simba, hivyo kuchagua mwenendo usioridhisha wa timu hiyo, hasa kwenye mechi zake za msimu huu wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Simba imepoteza zote mbili za hatua ya makundi, ambapo ilifungwa na Petro de Luanda (1-0) na Stade de Mallien (2-0).
Akizungumzia hilo, Mangungu amekanusha kile kinachoelezwa kuwa chanzo cha mwenendo mabovu huo ni migogoro kati ya upande wa Mwekezaji, Mohamed ‘Mo’ Dewji, na ule wa wanachama.
“Wanasema kuna mgogoro kati ya upande wa klabu na mwekezaji. Mimi na mwenyekiti wa bodi tunaongea kila mara, kama ni Mo mimi mara ya mwisho niliongea nae jana saa 8,” amesema.


