21.7 C
New York

Miji yenye watu wengi zaidi duniani

Published:

Na mwandishi wetu, Gazetini

MWAKA 1950, Tokyo (Japan) na New York (Marekani) ndiyo miji iliyokuwa na idadi kubwa ya watu duniani. Tokyo ilikuwa na watu milioni 12.6, huku New York ikiwa na milioni 9.3.

Kati ya miji 15 iliyokuwa na watu wengi wakati huo, nusu ilikuwa ya Bara la Ulaya au Amerika. Miji hiyo ni pamoja na London (milioni 7.9), Moscow (milioni 5.5) na Paris (milioni 5.4).

Kufikia mwaka 2000, Asia ikawa inaongoza kwa miji yake kuwa na watu wengi. Tokyo ikaendelea kuwa kinara kwa kufikisha watu milioni 30.3, wakati huo New York ikifikisha watu milioni 18.

Kwa sasa, mambo yamebadilika na Jakarta (Indonesia) ndiyo Mji unaoongoza duniani ukiwa na watu milioni 41.9, ukifuatiwa na Dhaka (Bangladesh) wenye watu milioni 36.6.

Aidha, Tokyo umeporomoka hadi nafasi ya tatu ukiwa na watu milioni 33.4 na chini yake ni New Delhi (India) wenye watu milioni 30.2.

Katika nafasi ya tano na sita ni miji miwili ya China, Shanghai (milioni 29.6) na Guangzhou (milioni 27.6).

Cairo (Misri) uko nafasi ya saba kwa watu milioni 25.6, ukifuatiwa na Manila (Ufilipino) wenye watu milioni 24.7. Mji wa Kolkata (India) unashika nafasi ya nane kwa watu milioni 22.5, kisha Seoul (Korea ya Kusini) ukiwa na watu milioni 22.5.

Miji mingine na idadi ya watu wake kwa sasa ni kama ifuatavyo; Karachi wa Pakistan (milioni 21.4), Mumbai nchini India (milioni 20.2), Sao Paulo wa Brazil (milioni 18.9), Bangkok wa Thailand (milioni 18.2), na Mexico City (milioni 17.7).

Related articles

Recent articles