13.1 C
New York

Mwamuzi kutoka Misri kuchezesha Dabi ya Kariakoo

Published:

Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Ligi Kuu  Tanzania Bara imemtangaza mwamuzi Amin Omar kutoka Misri kuwa mwamuzi wa kati wa mchezo wa Dabi ya Kariakoo, Yanga dhidi ya Simba, utakaopigwa  keshokutwa Juni 25, 2025  kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.

Mwamuzi  huyo  ataisaidiwa na Mahmoud Ahmed, Samir Gamal Saad, mwamuzi wa akiba ni Ahmed Mahrous Elghandour wote kutoka Misri, wakati Kamishna wa mechi NI Salim  Singano kutoka Tanga na mtathini waamuzi ni  Alli Mohamed kutoka Somalia.

Mchezo huo utakaopigwa saa 11:00 jioni, ndio utaamua bingwa wa msimu 2024/25 ambapo kwa sasa  Simba na  Yanga  zimepishana  pointi moja.

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img