Na Mwandishi Wetu
Klabu ya Mbeya City imefanikiwa kusalia Ligi kuu ya soka ya NBC Tanzania bara kufuatia ushindi wa jumla wa 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons kwenye michezo miwili ya mchujo (playoff) wa kusalia Ligi kuu.
Mbeya City iliibuka na ushindi wa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza kabla ya kutoshana nguvu kwa sare tasa kwenye mchezo wa pili uliopigwa leo Julai 8,2026, dimba la Sokoine, Mbeya huku Prisons wakielekea kwenye mchujo wa pili dhidi ya timu ya Polisi Tanzania kutoka Championship ili kujinusuru kushuka daraja.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mchezo huo, Kocha wa Mbeya City, Salim Mayanga amesema wamejifunza kutokana na changamoto walizokutana nazo na wanachosubiri ni mabadiliko kwa ajili ya msimu ujao.
“Timu itafanya marekebisho kwenye maeneo yote yaliyokuwa na udhaifu mkubwa msimu huu. Kutakuwa na ulazima wa kuongeza wachezaji wenye uwezo kwenye maeneo ambayo yalionekana kuwa na mapungufu makubwa,” amesema Mayanga.
Aidha Mayanga ametoa shukrani zake kwa mashabiki wa Mbeya na uongozi wa timu kwa ushirikiano wao, huku akiahidi kuwa wataendelea kufanya tathmini ya kina kuhusu kiwango cha ushindani wa ligi na jinsi ya kuleta mabadiliko chanya ndani ya kikosi hicho.


