Na Mwandishi Wetu, Gazetini
Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limemteua Mtanzania, Baraka Kizuguto kuwa Mratibu Mkuu wa michezo ya nusu fainali ya hatua za awali za kufuzu Kombe la Dunia Kanda ya Afrika kati ya Nigeria na Gabon na fainali.
Taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imefafanua kuwa Kizuguto atasimamia mechi zilizopangwa kufanyika jijini Rabat, Morocco Novemba 13 na Novemba 16, 2025.
Mshindi wa mchezo baina ya Gabon na Nigeria ataingia hatua ya fainali ya mashindano hayo ambapo atakutana na mshindi wa mchezo baina ya Cameroon na DR Congo.


