11.6 C
New York

Sheikh Ponda atangaza  rasmi kuwa mwanachama mpya ACT Wazalendo

Published:

Na Mwandishi Wetu

Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, leo Alhamisi Juni 5, 2025, ametangaza kujiunga na Chama cha ACT-Wazaendo, katika hafla iliyofanyika Magomeni, jijini Dar es Salaam.

Sheikh Ponda, ametangaza uamuzi wake wa kujiunga na ACT Wazalendo mbele ya umati wa wafuasi na viongozi wa chama hicho,  huku akisema  lengo ni kuhakikisha utawala  wa sheria,uchaguzi huru na wa haki unapatikana.

Amesema  ameona umuhimu wakuunga mkono  oparesheni  ya ACT Wazalendo ya ‘Linda Demokrasia’,  akisisitiza kuwa Taifa lolote linastahili  kuongozwa katika  misingi ya sheria  kwa kila  mtu bila kujali cheo  wala kabila.

Aidha ametoa wito kwa vijana, wanawake, wazee, na viongozi wa dini kuungana katika uwanja wa mapambano ya kudai haki mbalimbali zikiwemo za kisiasa kama vile kuhakikisha kura zetu zinahesabiwa kwa haki na viongozi wanaochaguliwa na wanawakilisha matakwa ya wananchi.

‘Kwa hiyo ndugu zangu  mimi nimeamua  kujiunga  ACT Wazalendo sio kwa sababu tu za kisiasa, mimi nimeamua kujiunga nikiamini kwamba katika jukwaa hili ule  uhuru wa kufanya zile harakati za kupambania haki za wanadamu  unapatikana,” amesema Sheik Ponda.

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img