12.7 C
New York

Konate kulamba mkataba mpya Liverpool

Published:

MERSEYSIDE, Uingereza
MABOSI wa Liverpool wamempa ofa ya mkataba mpya beki wake wa kati raia wa Ufaransa, Ibrahima Konate.
Hatua hiyo ya Liverpool inakuja wakati huu mlinzi huyo akihusishwa na vigogo wa La Liga, Real Madrid.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26, atamaliza mkataba wake wa sasa ifikapo mwishoni mwa msimu huu.
Wakati huo huo, winga wa kikosi hicho, Federico Chiesa, huenda naye akaondoka Afield ifikapo Januari, mwakani.
Klabu zinazotajwa kumpigia hesabu Muitalia huyo mwenye umri wa miaka 28 ni Inter Milan, Napoli, AS Roma na AC Milan.
Kwa upande mwingine, bado Liverpool inahusishwa na mpango wa kumsajili nahodha wa Crystal Palace, Marc Guehi.

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img