5.9 C
New York

Waziri Simbachawene  aagiza Jeshi la Polisi  kukamata watuhumiwa kwa staha

Published:

Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene, amemuagiza  Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Camillus Wambura kuhakikisha ukamataji wa watuhumiwa unafanywa kwa kufuata taratibu za kisheria na staha.

Pia amezuia Polisi kufanya ukamataji  wakiwa wamevaa vifunika uso ( kininja)  bila sare na wakiwa na silaha kubwa na ufanyike  mchana  kwa taarifa za  wazi .

Akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 8, 2025 jijini Dar es Salaam, Waziri Simbachawene amesema ukamataji usifuata sheria unazua hofu kwa familia za watu wanaokamatwa.

“Ukamataji  ninaoutaka mimi ni ule wa kisheria, askari anaenda anaripoti kwa mjumbe, mtu anajulikana yupo kazini kwake kwa nini uende  kumkamata nyumbani kwake ukiwa umevaa kininja? Tumekubaliana kwamba kuwe na ukamataji wenye  staha,” amesema.

Aidha amekosoa tabia ya kukamata watu kwa makosa madogo kama  kuposti  posti ndogo mitandaoni, akisisitiza kuwa vitendo hivyo vinachochea chuki dhidi ya Polisi wakati Jeshi hilo ndilo linahakikisha usalama wa wananchi

Waziri  huyo  ametoa angalizo  kwa wananchi kutoshiriki kile kinachoelezwa kama maandamano ya amani yasiyo na mipaka wala mwisho yanayohamasishwa mitandaoni na katika maeneo mbalimbali nchini.

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img