10.5 C
New York

Aston Villa wamfungia kazi Abraham

Published:

LONDON, Uingereza

KLABU ya Aston Villa haijarudi nyuma katika mkakati wao wa kumsajili mpachikaji mabao wa zamani wa Chelsea, Tammy Abraham.

Nyota huyo wa kimataifa wa England mwenye umri wa miaka 28, kwa sasa anacheza Bestikas kwa mkopo akitokea AS Roma.

Abraham amekuwa kwenye kiwango bora akiwa na Besiktas, ambapo amefunga mabao 13 katika mechi 26 alizowatumikia Waturuki hao.

Mbali ya huyo, pia kocha wa Villa, Unai Emery, hajaacha kumtolea macho straika wa Crystal Palace, Jean-Philippe Mateta.

Hivi karibuni, Emery alimrejesha winga raia wa Jamaica, Leon Bailey, ambaye alikuwa kwa mkopo AS Roma.

Kwa Abraham, itakuwa mara yake ya pili kuitumikia Villa kwani alifanya hivyo msimu wa 2018-19 akitokea Chelsea.

Katika mechi 40, aliifungia Villa jumla ya mabao 26 na kuiwezesha kurejea Ligi Kuu kupitia ‘play-off’ ya Championship.

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img