4.3 C
New York

Boti  ya mirungi kutoka Kenya yanaswa Tanga

Published:

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga, limekamata boti aina ya fibre, iliyokuwa ikisafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi kutoka nchini Kenya kupitia Bahari ya Hindi.

 Boti hiyo imekamatwa   wakati wa operesheni ya Polisi usiku wa Julai 22,2025, katika eneo la Mawe Mawili, Kijiji cha Kwale, mpakani mwa Wilaya ya Mkinga na Jiji la Tanga.

Akithibitisha tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, ACP Almachius Mchunguzi, amesema kuwa boti hiyo ilikamatwa na Kikosi cha Polisi Wanamaji,  kufuatia taarifa za kiupelelezi na ufuatiliaji wa kina wa mbinu zinazotumiwa na wasafirishaji haramu.

Kwa mujibu wa Kamanda Mchunguzi, watuhumiwa wawili waliokuwa kwenye boti walifanikiwa kutoroka baada ya kufika karibu na fukwe, lakini boti pamoja na shehena ya mirungi vilikamatwa.

Jeshi la Polisi  mkoani humo  limeeleza kuwa litaendelea kuimarisha doria na operesheni maalum hususan katika maeneo ya baharini ambayo yamekuwa yakitumiwa na wahalifu kuvusha bidhaa haramu kutoka nchi jirani.

Aidha, Kamanda Mchunguzi ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa mapema kuhusu viashiria vyovyote vya uhalifu katika jamii,  hasa vinavyohusiana na usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya.

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img