23.5 C
New York

Simba  ndoto zao ni kucheza  dabi, yawaita mashabiki kwa Mkapa Juni 15

Published:

Na Mwandishi Wetu

Pamoja na mkanganyiko uliopo juu ya mchezo dabi ambapo  Yanga wameweka wazi kuwa hawatapeleka timu uwanjani Juni 15, klabu ya Simba imetoa taarifa ya kuwaita mashabiki wao kwenda kujaza uwanja siku hiyo wakisisitiza kuwa mechi hiyo itachezwa.

Kwa  mujibu wa taarifa hiyo, iliyotolewa leo Juni 10,2025  mchezo namba 184 wa Ligi Kuu  dhidi ya Yanga uliopangwa kufanyika Juni 15, 2025 upo kama ulivyopangwa.

Uongozi wa klabu hiyo  umewataka wale ambao walinunua tiketi za mechi ya Machi 8, 2025 wazitunze kwa ajili ya matumizi ya mchezo huo na wale ambao hawajanunua tiketi wajiandae kununua baada ya tangazo la Bodi ya Ligi.

“Twendeni tukaujaze Uwanja wa Mkapa. Inafahamika wazi kuwa Ligi Kuu ya NBC inajumuisha Timu 16 na si ligi ya timu moja, kwa mujibu wa taratibu kabla ya kuanza msimu vilabu vyote16 hushiriki vikao na kutoa mapendekezo ya kuboresha kanuni na taratibu ili kuimarisha ligi yetu, hivyo wenye hoja wafuate taratibu husika,” imesema taarifa hiyo ya Simba na kuongeza kuwa

“Tunaomba Bodi ya Ligi na TFF watoe hadharani ripoti ya uchunguzi juu ya wale wote waliohusika kuharibu mechi ya ligi jioni ya tarehe 7/3/2025 na wachukuliwe hatua stahiki na mamlaka husika.

‘Kutotolewa kwa ripoti na kutochukuliwa hatua kwa wanaoendelea kuchochea ghasia ni sawa na kulinda uharamia katika mpira ambao unatia dosari mafanikio yaliyopo katika tasnia ya mpira wa miguu nchini kwa sasa.”

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img