21.1 C
New York

TFF kumpata mshirika wa ‘kubeti’

Published:

Na Mwandishi Wetu

Shirikisho wa Soka Tanzania(TFF),limesema kuanzia msimu ujao wa 2025/2026 litakuwa na mshirika wa michezo ya kubashiri(kubeti) katika mashindano yake yote.

Kwa mujibu wa taarifa ya TFF  waliyotoa leo, Mei 12, 2025 mshirika huyo atashikilia haki hizo kwa kipindi chote cha makubaliano, hivyo yeyote mwenye nia au kuhitaji ‘Odds’ kwa ajili ya mechi ambazo zitakuwa chini ya TFF atalazimika kuwasiliana na mshirika huyo.

“Makubaliano yetu na mshirika huyo yatakuwa ni kwa ajili ya odds tu na si ushirika mwingine na kampuni za michezo ya kubashiri(betting companies) kama udhamini(sponsorship) au ushirikiano,” imesema taarifa hiyo kwa umma.

Taarifa hiyo imesema kuwa utaratibu huo ndio unaotumika katika ligi mbalimbali barani Ulaya, ikieleza kuwa itazinufaisha kimapato klabu mechi zao zitakuwa zimeingia kwenye odds.

“Licha ya malipo yatakayokuwa yanatokana na odds, bado klabu zitaendelea kudhaminiwa na kampuni hizo michezo ya kubashiri, kwani utaratibu huu hauathiri makubaliano ya udhamini kati ya pande hizo.

“Utaratibu wa kumpata mshirika huyo utafanyika kwa njia ya mnada utakaotangazwa  wakati wa utakapowadia,” imesema.

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img