30 C
New York

Serengeti Boys kuandika historia nyingine Kombe la Dunia?

Published:

Na mwandishi wetu, Gazetini

BAADA ya kufika fainali ya AFCON kwa vijana wa U-17, Serengeti Boys itashiriki michuano ya Kombe la Dunia kwa vijana wa umri huo itakayofanyika mwishoni mwa mwaka huu huko Qatar.

Mashindano hao ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) yataanza rasmi Novemba 19 hadi Desemba 13, 2026, yakishirikisha mataifa 48 na Qatar inakuwa mwenyeji wa michuano hiyo kwa mara ya pili mfululizo.

HAKUNA BINGWA MTETEZI

Fainali za mwaka huu hazina bingwa mtetezi baada ya vijana wa U-17 ya Ureno kushindwa kufuzu. Hata hivyo, vigogo Brazil, Argentina na Hispania watakuwa sehemu ya michuano.

Makundi 12 yenye timu nne kila moja yatazalisha jumla ya mechi 104 kwa kipindi chote cha mashindano hayo.

FURSA ZAIDI KWA SERENGETI BOYS

Baada ya kile walichokionesha AFCON, kuingia kwa mara ya kwanza hatua ya fainali, Kombe la Dunia la U-17 ni jukwaa jingine kubwa kwa vijana wa U-17 kutangaza vipaji vyao duniani.

Msimu uliopita, jumla ya maskauti 130 kutoka klabu kubwa za soka barani Ulaya na duniani kwa ujumla walifika Qatar kufuatilia mashindano hayo.

KUVUKA MAKUNDI?

Serengeti Boys iko Kundi I, ambalo pia lina vijana wenzao wa U-17 kutoka katika mataifa ya Brazil, Jamhuri ya Ireland na Costa Rica.

Katika makundi 12, timu mbili zitakazomaliza nafasi za juu zitaingia hatua inayofuata ya 32 Bora, zikiongozana na zingine nane zitakazoshika nafasi ya tatu zikiwa na takwimu nzuri (best loser).

Related articles

Recent articles