22.9 C
New York

Visual| Ushamiri wa VVU nchini Tanzania

Published:

Hali ya Ushamiri kwa kila Mkoa(%)

Tanzania inaendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuhakikisha kuwa inatokomeza janga la UKIMWI kufikia mwaka 2030 kama ilivyo pia katika malengo ya Kimataifa ya kuondokana na janga hilo.

Wakati jitihada hizo zikiendelea gazetini.co.tz imeangazia hali ya ushamiri wa maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI nchini Tanzania kwa kila mkoa.

Katika takwimu hizo ambazo zimetolewa na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) zilizoangazia utafiti wa mwaka 2003/2004, 2007/2008, 2011/2012 na 2017/2018 zinaonyesha kuwa mikoa ya Dodoma, Tanga, Morogoro, Iringa, Kagera, Mwanza na Manyara kuwa na kiwango cha juu cha ushamiri.

Kwa mujibu wa TACAIDS hii inawezekana ni matokeo ya mambo mawili ya msingi ambayo kwanza ni kuongezeka kwa maambukizi mapya au kuimarika kwa huduma za matibabu ya UKIMWI ambapo watu wanaishi muda mwingi.

Zaidi unaweza kutazama picha halisi ya viwango vya ushamiri kwenye usanifu wetu.

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img