16.3 C
New York

Rais Samia aongeza kima cha chini cha mshahara, sasa ni Sh 500,000

Published:

Na Mwandishi Wetu, Gazetini

Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan ametangaza kuongeza   kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma kwa  asilimia 35.1 mwaka 2025 ambapo kwa sasa kima cha chini kitapanda kutoka 370,000 hadi 500,000.

Amesema hayo leo  Alhamisi Mei 1,2025  kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi  yaliyofanyuka Kitaifa mkoani Singida.

Rais  Samia amesema wafanyakazi wamekuwa na mchango mkubwa katika kuinua uchumi wa nchi na ataendelea kuboresha maslahi ya watumishi hao.

“Sasa kwa kuwa mcheza kwao hutunzwa, mimi na wenzangu baada ya kuangalia uchumi ulivyopanda na umepanda kwa sababu ya nguvu zenu wafanyakazi, ninayo furaha ya kuwatangazia kwamba mwaka huu Serikali itaongeza kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma kwa 35.1%, amesema.

Ameeleza kuwa ngazi nyingine za mshahara nazo zitapanda kwa kiwango kizuri jinsi bajeti inavyoruhusu, huku akisema bodi inaendelea kufanya mapitio ili kuboresha viwango vya chini vya mshahara kwa wafanyakazi wa sekta binafsi.


Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img