27.4 C
New York

Jeshi la Polisi lataja sababu ya kumkamata kiongozi wa Chadema

Published:

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limemkamata Naibu Katibu Mkuu  Bara wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Aman Golugwa kwa uchunguzi wa tuhuma za kusafiri kwa siri kwenda na kurudi nje ya Tanzania.

Taarifa ya Jeshi la Polisi iliyotolewa  leo  Mei 13, 2025 imesema Golugwa amekamatwa saa 6:45 usiku Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, akiwa katika maandalizi ya kusafiri kuelekea Brussels nchini Ubelgiji.

“Jeshi la Polisi lilimkamata Naibu Katibu Mkuu huyo kufuatia taarifa za siri kuwa amekuwa na mienendo ya kuondoka na kurudi nchini bila kufuata taratibu za kisheria hapa nchini,”

“Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linaendelea na uchunguzi wa kina wa taarifa hizi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama kuhusu suala hilo.”

Katika taarifa hiyo, Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wananchi kuendelea kuwa watulivu wakati uchunguzi ukiendelea na kupuuza taarifa za upotoshaji kuhusu hatua hizi za kisheria zinazomuhusu Golugwa.

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img