23.1 C
New York

Bosi DRFA afungiwa  na TFF miaka sita

Published:

Na Mwandishi Wetu, Gazetini


Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA),Ramadhan Missiru amefungiwa na Kamati ya Maadili ya Soka Tanzania (TFF), kutojihusisha na shughuli zozote za mpira wa miguu kwa kipindi cha miaka sita ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa taarifa ya TFF iliyotolewa leo Mei 13, 2025 na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano, Clifford Ndimbo, Missiru alipatikana na hatia ya makosa mawili ya ukiukwaji wa maadili yaliyobainishwa na kamati hiyo katika kikao chake kilichofanyika Mei 8, 2025 jijini Dar es Salaam.

Taarifa hiyo imesema kuwa Missiru alishtakiwa na Sekretarieti ya TFF kwa makosa mawili ikiwemo kushindwa kutii maamuzi ya Kamati ya Maadili, kinyume na Kanuni ya 73(8) ya Maadili ya TFF Toleo la 2021. Kosa lingine ni kuchochea umma, kinyume na Kanuni ya 73(4) ya Maadili ya TFF Toleo la 2021.

“Baada ya Kamati kusikiliza pande zote na kupitia nyaraka na vielelezo vilivyowasilishwa mbele yake. imemtia hatiani kwa makosa mawili na kumpa adhabu ya kumfungia  kijihusisha na masuala ya mpira wa miguu  ndani na nje ya nchi kwa kipindi cha miaka sita na kulipa faini ya sh 5,000,000,”

Kwa upande wa Mkuu wa Idara ya Habari ya na Mawasiliano ya Klabu ya Azam, Thabit Zakaria ‘Zakazakazi’, aliyeshtakiwa katika kamati hiyo kwa kuchochea umma, kamati ilibaini hakuna ushahidi wa kutoasha kumtia hatiani.

Related articles

spot_img

Recent articles

spot_img